Monday, 21 September 2015

Hii ni Top 10 ya warembo wa mastaa wa Ligi Kuu soka Uingereza 2015

Tumezoea kuona mastaa kadhaa wa soka kuingia katika headlines na wapenzi wao, wakiwa wametoka out katika sehemu mbalimbali za starehe baada ya kazi nzuri walioifanya uwanjani. Stori kutoka talksport.com waliwahi kutoa May 2015 list ya Top 10 ya warembo wa mastaa wa soka wa Ligi Kuu Uingereza.
10- Edurne Garcia huyu ni mpenzi wa golikipa wa klabu ya Manchester United David de Gea.
edurne_getty
De-Gea1



9- Lorena Bernal huyu ni mke wa kiungo wa Arsenal Mikel Arteta
lorenabernal_getty
bernal-and-arteta
8- Anara Atanes huyu ni mpenzi wa kiungo wa klabu ya Manchester City Samir Nasri
275CB7BF00000578-3030034-image-m-13_1428482498503
anara-atanes-et-samir-nasri-exact-353970864
7- Helen Flanagan mpenzi wa staa wa soka wa klabu ya Aston Villa Scott Sinclair
flanagangetty
C_71_article_1461799_image_list_image_list_item_1_image
6- Coleen Rooney mke wa mshambuliaji na nahodha wa klabu ya Manchester United Wayne Rooney
rooney_getty
English soccer player Wayne Rooney and his girlfriend Colleen McLoughlin arrive for the FIFPRO World X1 Player Awards at the BBC TV centre, London, Monday Sept. 19, 2005.  The awards are taking place for the first time, and are the first  soccer awards voted by professionals from across the world.  (AP Photo/Kirsty Wigglesworth)
5-  Sam Cooke mpenzi wa beki wa kati wa klabu ya Manchester United Chris Smalling
sam-cooke
cooke_getty
4- Georgina Dorsett mpenzi wa kiungo wa zamani wa timu ya Manchester United na Everton Tom Cleverley
dorsett_getty
b93394d8f669b427f347c7afef75d5f4
3- Ludivine mrembo wa beki wa zamani wa klabu ya Arsenal na Manchester City Bacary Sagna
sagnagetty
France's defender Bacary Sagna and Ludivine Sagna enjoy a day out on a beach in Rio de Janeiro during the 2014 FIFA World Cup on June 26, 2014. AFP PHOTO / FRANCK FIFE        (Photo credit should read FRANCK FIFE/AFP/Getty Images)
2- Abbey Clancy mrembo wa mshambuliaji wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Stoke City Peter Crouch
gettyimages-452325248
Abbey-Clancy-and-Peter-Crouch
1- Misse Beqiri mrembo wa golikipa wa zamani wa Man United ambaye ametimkia West Bromwich Albion msimu huu Anders Lindegaard.
Misse-Beqiri

Baada ya siku 40: sura ya mtoto wa Diamond na Zari ndio hii imeonyeshwa kwenye picha !

Zimeshatimia siku 40 toka mtoto wa Diamond Platnumz na Zarinah Hassan azaliwe, anaitwa Tiffah…. ambapo siku hii kubwa ilikumbukwa na nyumbani kwa Diamond watu mbalimbali wakaalikwa kama ilivyo kwenye utaratibu.
T2
T3
T1Picha zote 3 za juu ni kutoka kwenye Instagram page ya @8020fashions
T6
T7Ustaa wa Diamond Platnumz na Zari umeshawishi mpaka kampuni kubwa za kibiashara kuingia mkataba wa malipo kutumia jina na picha za Tiffah kibiashara ambapo mtoto huyu ambaye ndio kwanza katimiza siku 40 za kuzaliwa, tayari ni balozi wa maduka ya nguo za watoto Dar es salaam lakini pia picha yake ya kwanza imeonyeshwa ikiambatana na udhamini wa benki.
t9
t8

Mtoto wa Beckham amelikataa soka? Haya ndio maneno yaliyomuumiza baba yake

David Robert Joseph Beckham ni staa wa Soka ambaye kastaafu Soka na kuacha Rekodi kubwa na nzuri zinazoheshimika Duniani, yako maneno kwamba maji hufuata mkondo, mtoto wa Beckham na Soka la Baba yake je?
Stori ni vice versa, David Beckham kathibitIsha kwamba mtoto wake na Mchezo wa Mpira wa Miguu hata haviendani >>> “Mwanangu mmoja aliniambia kwamba haoni kama atakuja kuwa Mchezaji wa Mpira wa Miguu kwenye maisha yake, ilinivunja moyo kwa upande mwingine“- David Beckham.
BECKHAM_main_1473299a
Beckham akiwa na Familia yake kwenye matembezi yao.
Kwenye sentensi nyingine Beckham anasema mtoto wake ana hofu kwamba wapo watakaolinganisha kiwango chake na baba yake >>> “Kila nikiingia uwanjani najua watu wanasema ‘yule ni mtoto wa Beckham’, nisipokuwa na kiwango kizuri kama wewe hata haipendezi“- David Beckham.
David-and-his-sons

Tyga matatani na malimbukizi ya kodi, makosa ya kuvunja mkataba & wizi…!!





Hiko sio kitu pekee ambacho Jimbo la Carlifonia linataka kutoka kwa rapper huyo, mwezi uliopita Mahakama ilimuamuru Tyga kumlipa mwenye nyumba wa nyumba aliokuwa anaishi kodi ya nyumba ya miezi miwili ambacho kiasi chake kiligonga Milion 140 kwa pesa ya Kitanzania.
tyga6
Muonekano wa ndani wa duka la Tyga ‘Last Kings’.
Mengine ambayo Jimbo hilo linashitaki dhidi ya Rapper huyo wa Cash Money Records ni kesi ya kuvunja mkataba wake na moja ya club ya Las Vegas, mkataba ulikuwa wa dola 100,000 na ulikuwa unasema kwamba Tyga hatokuwa na mamlaka ya kuperfom sehemu yoyote ile Las Vegas isipokuwa club ya ‘Body English’ jijini humo, Tyga alivunja mkataba huo ambao kwa shilingi ya Kitanzania tunazungumzia makubaliano yaliozidi Milion 200 kwa kwenda kutoa show kwenye club nyingine jijini Las Vegas!

Sunday, 1 February 2015

Amuua mke kwa kumkata kichwa gesti

1st February 2015
Mkazi wa Tabata Mawenzi, Remi Joseph (36) anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuua mkewe kwa kumkata kichwa kwenye nyumba ya wageni ya Friends Corner ya jijini Dar es Salaam.
Aliyeuawa ni Josephena Moshi (35), ambaye alikatwa kichwa na kuchomwa na kitu chenye ncha kali kifuani wakiwa kwenye nyumba ya wageni ya Friends Corner.

Akihojiwa kuhusiana na tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa  Kinondoni, Augustine Senga, alikiri kutokea mauaji hayo.
Alisema kuwa tukio hilo lilitokea Alhamisi saa 8:00 mchana na kwamba familia hiyo ilikuwa inaishi Tabata Mawenzi.

Senga alisema mwanamke huyo alifariki papo hapo baada ya kushambuliwa na kwamba chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika na uchunguzi unaendelea.
Kamanda Senga alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili na mtuhumiwa anashikiliwa na polisi.

Hata hivyo, mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa baada ya mtuhumiwa huyo kufanya mauaji hayo, alifanya jaribio la kutaka kujiua lililoshindikana.

Kamanda alipoulizwa kuhusiana na mtuhumiwa huyo kutaka kujiua, alisema kuwa uchunguzi unaendelea.

“Bado ni mapema sana kueleza kila kitu hayo niliyokueleza ni taarifa za awali kwani na huyu mtuhumiwa amekutwa na majeraha shingoni, hivyo masuala ya kazi yake na sababu vinachunguzwa,” alisema Senga.

MKUU WA MKOA AFUNGUA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MITANDAO YA KIJAMII

01_0567b.JPG
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Elimu Zanzibar (ZEDO) Ussi Said Suleiman akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdallah Mwinyi Khamis katika ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya Social Media huko Chuoni kwao Mwanakwerekwe Mjini Zanzibar.Picha na Makame Mshenga wa Maelezo Zanzibar.
02_ccda3.JPG
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdallah Mwinyi Khamis (alie simama) akiwahutubia washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya matumizi ya Mitandao ya kijamii (Social Media), hawapo pichani yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Maendeleo ya Elimu Zanzibar kwa kushirikiana na Kigamboni Community Centre KCC kutoka Dar es Salam, huko Chuoni kwao Mwanakwerekwe Mjini Zanzibar.Picha na Makame Mshenga wa Maelezo Zanzibar.
03_68a56.JPG
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakimskiliza Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdallah Mwinyi Khamis (hayupo pichani).
04_0d2c4.JPG
Mgeni rasmin Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdallah Mwinyi Khamis (wakatikati) waliokaa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya matumizi ya Mitandao ya kijamii (Social Media).Picha na Makame Mshenga wa Maelezo Zanzibar.

SIMBA YAPIGWA FAINI YA MILIONI 3/-

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeipiga klabu ya Simba faini ya sh. milioni tatu kutokana na timu yake kuvaa jezi ambazo hazikuwa na nembo ya mdhamini wa Ligi Kuu, kampuni ya Vodacom wakati wa mechi yao dhidi ya Kagera Sugar.
Mechi hiyo namba 50 ya Ligi Kuu ya Vodacom ilichezwa Desemba 26 mwaka jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 13(7) ya Ligi Kuu inayotaka klabu kuheshimu masharti ya udhamini wa Ligi Kuu kwenye mechi zake.
Nayo Polisi Tabora imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa mujibu wa kanuni ya 28(4) kwa kusababisha mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati yake na Toto Africans iliyochezwa Januari 14 mwaka huu Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kuvurugika.
Kutokana na mchezo huo kuvurugika, Toto Africans imepewa ushindi wa pointi tatu na mabao matatu. Uamuzi huo umefanywa kwa kuzingatia kanuni ya 28(1) inayotawala ligi hiyo

Saturday, 31 January 2015

Mtaalamu wa silaha za kemikali IS auwawa






Jeshi la Marekani linasema kuwa mtaalamu mmoja wa silaha za kemilkali aliyekuwa akifanya kazi na kundi la Islamic State ameuawa kwenye mashambulizi ya muungano nchini Iraq.
Marekani inasema kuwa kifo cha mwanamume huyo kwa jina Abu Malik kitavuruga uwezo wa kundi hilo wa kuunda na kutumia silaha za kemikali.
Abu Malik anaripotiwa kufanya kazi kama mtaalamu wa silaha za kemikali kwa rais wa zamani wa Iraq Sadam Hussein kabla ya uvamizi ulioongozwa na Marekani mwaka 2003.
Kundi la Islamic State hudhibiti maeneo makubwa nchini Syria ambapo serikali imekuwa ikiharibu silaha za kemikali.

Lazaro Nyalandu na Aunt Ezekiel Wachanwa Bungeni!!!



Lazaro Nyalandu na Aunt Ezekiel  Wachanwa Bungeni!!!



 Jana wakati mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema , akichangia  hoja Bungeni nakudai kuwa mawaziri wengi  hawana ubunifu nakumrushia “bomu”  Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kuwa anazunguka nje ya nchi na msichana kwa madai ya kutangaza utalii.
Lema alisema;
“Angalia Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alikwenda kutangaza utalii nje ya nchi akiwa ameongozana na (mwigizaji maarufu wa filamu wa Tanzania) Anti Ezekiel,” alisema na kuongeza kuwa waziri huyo hashindi ofisini kwa kisingizio cha kutangaza utalii.
Picha za wawili hawa wakiwa nchini Marekani  wakitangaza utalii zilisambaa sana mtandaoni mwaka jana na kizua stori nyingi juu kile kilichofanyika.
Picha : Waziri Nyalandu akiwana Aunty Ezekiel pamoja na DJ Luke (wakatikati) wakitangaza Utalii, New York, Marekani.
Lakini hivi kuna ubaya gani Staa wetu kushirikiana na waziri katika kutangaza UTALIIII?!!



BARABARA YA KWENDA OLOLOSOKWAN YAWA TISHIO KWA MAGARI MAKUBWA

DSC_0035
Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyemtembelea ofisini kwake wakati wa ziara ya kikazi ya siku nne kwenye kijiji cha Ololosokwani na halmashauri ya Ngorongoro kwa ajili ya maandalizi ya mradi wa kijiji cha digitali unaoendeshwa na Unesco kwa kushirikiana na Ki-elektronic ya Samsung unaotarajiwa kuwasili kijijini hapo mwezi februari ukitokea jijini Dar.
MKURUGENZI Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues ameonesha mashaka yake juu ya ubora wa barabara ambazo magari mazito yenye vifaa vya kijiji cha digitali Ololosokwan yanaweza kupita.
Alisema hayo kwenye mazungumzo na Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro Elias Wawa Lali wakati alipomtembelea ofisini kwake. Akiwa katika ofisi za mkuu huyo wa wilaya kumwelezea shughuli za Unesco katika wilaya yake, Mkurugenzi Mkazi huyo alipata nafasi ya kuzungumzia haja ya kuboreshwa kwa maaneo kadha ya barabara kuelekea kijiji cha Olosokwan ili kuyawezesha magari hayo makubwa kufika kwa urahisi.
Huku akimuonesha mkuu wa wilaya baadhi ya picha alizopiga akiwa njiani kukagua njia ya kupita magari hayo na kuangalia maandalizi ya mwisho ya mradi huo mkubwa na wa kipekee nchini alisema hali ya barabara si nzuri hata kidogo. Vifaa kwa ajili ya kijiji hicho vipo bandarini tayari na magari yanayoweza kubeba makontena hayo ni makubwa na barabara za kuelekea kijiji hicho ni mbaya.
DSC_0041
Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali (katikati) akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (kulia) aliyeambatana na wataalamu wa elimu, afya na mawasiliano pamoja na Mratibu wa Taifa wa tiba asilia na mbadala katika Idara ya Tiba Wizara ya Afya na ustawi wa jamii. Dkt Liggy Vumilia (hayupo pichani) .
                                                                                                 VICTOR SIMON

PAC YAISHAURI SERIKALI NAMNA YA KUINUSURU KAMPUNI YA TTCL

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deo Filikunjombe wakiwa katika majukumu yao.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deo Filikunjombe wakiwa katika majukumu yao.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) akiwa katika majukumu.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) akiwa katika majukumu.
KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imetoa mapendekezo ya kuinusuru Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kutokana na hali mbaya ya kampuni hiyo kifedha kwa sasa ambapo inaendeshwa kwa hasara huku ikiwa na madeni makubwa. PAC imetoa mapendekezo hayo katika taarifa yao kwa bunge ya mwaka juu ya ukaguzi wa hesabu za Serikali kwa mashirika ya umma iliyotolewa Januari 28 mwaka 2015.
Kwa mujibu wa taarifa ya PAC hali ya mapato na matumizi ya TTCL kwa mwaka 2012 ilipata hasara ya bilioni 20.883 huku kwa mwaka 2013 ikipata hasara ya bilioni 16.258. PAC ilisema majumuisho ya hasara ya TTCL kupata hasara kwa takribani kwa miaka 10, Kampuni sasa imekuwa na hasara ambayo kwa mwaka 2013 ilifikia bilioni 334.48, jambo ambalo limeiondolea mvuto wa kukopeshwa na taasisi za fedha hata zile zenye nia ya kuikopesha.
"...Ukosefu wa fedha za kutosha kutekeleza miradi ya Kampuni umekuwa kikwazo kwa TTCL kukabiliana na ushindani wa kibiashara. Kwa kipindi kirefu ufanisi wa TTCL kiuwekezaji na kifedha umeendelea kudorora. Tangu TTCL ibinafsishwe mwaka 2001, hakuna uwekezaji mkubwa uliofanyika na mpango wa kutafuta mkopo kutoka mabenki ya ndani na nje ya nchi unakwamishwa na masharti ya kupata udhamini wa Serikali," ilieleza taarifa hiyo ya PAC. PAC iliongeza kuwa ukiacha madeni yaliopo pia TTCL inadaiwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) jumla ya bilioni 25 hivyo kufanya jumla ya deni kufikia bilioni 101.6.
Kamati hiyo ya bunge imesema kuna umuhimu wa Serikali kufanya maamuzi ya haraka ya kuikwamua TTCL ili iweze kuendelea kutoa huduma kwenye Sekta ya Mawasiliano ikizingatiwa kuwa ndiyo inayoendesha Mkongo wa Taifa wa mawasiliano. Katika mapendekezo ya PAC ili kuikwamua TTCL imeishauri Serikali kununua hisa asilimia 35 zinazomilikiwa na Bharti Airtel katika TTCL kwa gharama ndogo kwani Bharti Airtel haikutimiza kikamilifu masharti ya mkataba wa mauziano ya hisa hizo hapo awali kwani tangu inunue hisa hizo haijafanya uwekezaji katika Kampuni ya TTCL.
"...TTCL isamehewe deni la Serikali Sh. 76.6 bilioni na deni la TCRA Sh. 25 bilioni ambayo jumla yake ni Sh. 101.6 bilioni na fedha hizo zipelekwe kuongeza mtaji ili Kampuni itoke kwenye kuwa na mtaji hasi wa Sh. 87.896 bilioni na kuwa na mtaji chanya wa sh. 13.704 bilioni. Likifanyika hili basi Kampuni hiyo itaweza kukopesheka. Serikali ikamilishe taratibu zake za kuimilikisha TTCL Mkongo wa Taifa ili izidi kuuendeleza kwa ufanisi na kuongeza mapato ya TTCL," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo. Hata hivyo PAC imeshauri kuwa kuna umuhimu wa kufanya marekebisho ya muundo wa Kampuni ya TTCL kwani kwa sasa ina idadi kubwa ya wafanyakazi (1549) isiyoweza kuwalipa.
Aidha, ilibainisha kuwa kwa sasa zinahitajika bilioni 32 kwa ajili ya kugharamia urekebishaji wa muundo wa Kampuni ili uendane na mahitaji ya utoaji wa huduma mbalimbali. Mashirika mengine yenye hali mbaya kifedha na uendeshaji ni pamoja na Shirika la Ndege Tanzania, ATCL ambayo kwa sasa ina madeni makubwa huku ikiwa na ndege moja aina ya Dash 8–Q 300, Wafanyakazi 142 na Jengo la ATC House lililoko mtaa wa Ohio, Dar es Salaam.

BUNGENI: CHENGE ACHARUKA KUHUSU UFISADI


MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee (Chadema) ametakiwa kuwasilisha ushahidi kuthibitisha kauli yake ya kumtuhumu Mbunge Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), kwa ufisadi.
Chenge alilazimika kuomba utaratibu wa kiti juzi, baada ya Mbunge huyo wa Kawe kumtaja mara mbili wakati akichangia mjadala wa taarifa za kudumu za Bunge zilizowasilishwa juzi.
Mara ya kwanza, Mdee alimhusisha Chenge na mkataba mbovu wa Kampuni ya Ndege (ATCL) uliosababisha Serikali kuingia hasara ya zaidi ya Sh bilioni 90.
Licha ya kumtaja kwenye ufisadi huo ambao kwa mujibu wa Mdee, Chenge ndiye alikuwa Waziri wa Wizara yenye dhamana na ATCL, pia alimtaja kuhusika katika kashfa nyinginezo ikiwemo suala la utoaji takribani Sh bilioni 200, katika iliyokuwa Akaunti ya Tegeta Escrow ya Benki Kuu (BoT).(P.T)
"Wabunge tuanze kuchunguzana humu ndani na kushughulikiana,"alisema Mdee na kutaja kwamba kwa kuanza, waanze na Chenge pamoja na Dk Shukuru Kawambwa (Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi), akimhusisha kuwa aliwahi kushika wizara hiyo yenye dhamana na ATCL.
Kauli hiyo ilimfanya Chenge kusimama na kusema; "kwa heshima zote nimemvumilia sana mheshimiwa (Mdee) anayechangia hoja hii. Kama ana ushahidi wa hayo anayosema, kanuni zetu zinatutaka ayawasilishe mbele yako.
"Mimi ningelipenda Bunge hili liendelee kuwa na heshima yake. Pili naomba sana, hayo wanayoyasema wawe na ujasiri wa kwenda kuyasemea nje ya ukumbi huu wa Bunge, wasijifiche kwenye kinga ya Bunge.
"Nina mengi ya kusema, lakini kwa sababu nimesimama kwa hoja ya utaratibu, kunitaja moja kwa moja, naomba aweke hoja mezani,"alisema Chenge.
Mwenyekiti wa Bunge alikubaliana kwamba Mdee awasilishe ushahidi kwa kiti. Hata hivyo Mdee alijibu, "Kuna utaratibu wa kikanuni, vielelezo nikitakiwa kuleta nitaleta.
"Tunazungumza hapa matumizi mabovu, mikataba mibovu na wizi wa mali ya umma. Mzee wangu (Chenge) ni rafiki yangu lakini nimeamua nimfungukie kwa sababu haya ni mambo makubwa."

Friday, 30 January 2015

MUGABE ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA AU


Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ndio mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika -Au
Rais mkongwe wa Zimbabwe Robert Mugabe, mwenye umri wa miaka tisini, sasa ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa muungano wa Afrika-AU.
Wajumbe walimteuwa Mugabe kwa kauli moja katika mkutano wa AU unaoendelea mjini Addis Ababa-Ethiopia.
Sasa Mugabe amechukua mahala pak mwenyekiti anayeondoka wa muungano huo, Nkosazana Dlamini-Zuma.
Uteuzi wa Mugabe kuongoza muungano huo mkubwa ulio na wanachama zaidi ya arubaini, sasa umeingiza doa ndani ya AU, kwani Mugabe hana uhusiano mzuri na mataifa ya Magharibi, hasa baada ya kukaa uongozini tangu Zimbabwe ilipojipatia uhuru mnamo mwaka wa 80.BBC



.

Umoja wa Afrika: mshikamano dhidi ya Boko Haram

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Nkosazana Dlamini-Zuma ametangaza mjini Addis Ababa, Ethiopia kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kwa kuanzisha vita dhidi ya Boko Haram.
Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Nkosazana Dlamini-Zuma ametangaza mjini Addis Ababa, Ethiopia kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kwa kuanzisha vita dhidi ya Boko Haram.
Na RFI
Uamzi wa pamoja umechukuliwa na Umoja wa Afrika wakati wa kikao chake cha Baraza la amani na usalama Alhamisi Januari 29 jioni mjini Addis Ababa, Ethiopia na kuhudhuriwa na zaidi ya marais kumi na tano.
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan na rais wa Cameroon Paul Biya hawakushiriki kikao hicho. Umoja wa Afrika unaunga mkono kikosi cha kimataifa cha wanajeshi 7500.(P.T)
Lengo la Umoja wa Afrika ni kushawishi Umoja wa Mataifa kufadhili mashambulizi ya kikosi hicho cha Umoja wa Afrika.
Uamzi huo umechukuliwa na marais na viongozi wa serikali za Afrika Alhamisi 29 Januari mjini Addis Ababa, ambao wanakabiliwa na tishio la Boko Haram.
Mwezi ujao, Umoja wa Afrika utakutana rasmi na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, ili kuliomba kusaidia, kupitia mfuko wa amani, msaada wa vifaa na fedha kwa kikosi cha kimataifa chenye wanajeshi 7500, ambao watatakiwa, kwa mujibu wa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Nkosazana Dlamini-Zuma, kupambana dhidi ya Boko Haram.
Umoja wa Afrika unaunga mkono jitihada za jumuiya ya nchi zinazochangia Ziwa Chad, za kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kutoka Nigeria, Chad, Cameroo, Niger na Benin.
Uamzi huu umechukuliwa na zaidi ya marais kumi na tano ambao ni wajumbe wa Baraza la amani na usalama, uamuzi ambao unatazamiwa kupitishwa katika mkutano mkuu wa marais na viongozi wa serikali ambao utadumu siku mbili kuanzia Ijuma wiki hii.
Nigeria na majirani zake wameafikiana juu ya msimamo wa pamoja, baada ya miezi ya kutoaminiana na kutokuelewana. Lakini kama Umoja wa Afrika, kupitia jumuiya ya nchi zinazochangia ziwa Chad, una wanajeshi, bao unakabiliwa na ukosefu wa vifaa vya kijeshi na fedha.

SIMBA WAAMUA KUFANYA MAAMUZI MAGUMU


WAZEE wa Simba wameona isiwe taabu na wameamua kurudi kazini kwa kufanya kikao chao cha dharura na baadhi ya viongozi na jana Alhamisi jioni walituma ujumbe wao kambini kuzungumza na wachezaji kwenye kikao cha faragha kutaka kujua tatizo ni nini mbona timu inayumba?
Lakini si hilo tu, viongozi wa matawi ya Simba Dar es Salaam wameungana na kuuandikia barua uongozi wakishinikiza mambo matatu ambayo ni uamuzi mgumu, ambayo ni kuitisha mkutano wa dharura wa wanachama kujua tatizo la timu yao, kufumua benchi la ufundi abaki kocha Mserbia, Goran Kopunovic pekee na mwisho Kamati ya Mashindano ipigwe chini.
Wanachama hao chini ya kiongozi wao, Masoud Ustaadh, wanadai kwamba mambo hayo ndiyo tatizo na chanzo cha Simba kufanya vibaya kwenye Ligi Kuu Bara na kwamba viongozi wa kamati wamekuwa wakiingilia benchi la ufundi.(P.T)
Kwa mujibu wa maelezo yao, wanataka hata Selemani Matola apigwe chini kwa madai kwamba hata Kocha Patrick Phiri alishadokeza awali kuwa Kocha Msaidizi huyo hafai.
Rais wa Simba, Evans Aveva, amekiri kupokea barua hiyo na kusema anaifanyia kazi kwa mujibu wa Katiba ya Simba.
Tafrani hiyo imezuka baada ya timu hiyo kupigwa mabao 2-1 na Mbeya City juzi Jumatano kwenye mechi ya ligi hiyo ndani ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Wazee hao waliibukia kambini jana kutaka wachezaji wawaambie ukweli ambapo kikao hicho kilitumia saa kadhaa huku kukiwa na usiri mkubwa.
Mmoja wa wachezaji aliiambia Mwanaspoti baadaye kwamba baadhi yao walitamka kwamba walifungwa kwa makosa ya uwanjani, ingawa wengine walilalamika kuwa morali iko chini kwavile viongozi hawapo karibu nao.
Kocha aliyetimuliwa na Simba, Patrick Phiri kwa upande wake ameweka wazi kwamba timu hiyo ilikosea kuwaacha Amri Kiemba na Haroun Chanongo lakini akatoa angalizo kwamba Mserbia Kopunovic asiguswe, aachwe afanya kazi yake.
Phiri alitimuliwa Simba mwezi uliopita na nafasi yake kuchukuliwa na Mserbia huyo.
Akizungumza na Mwanaspoti jana kutoka Zambia, Phiri alionyesha kusikitishwa na matokeo ya Simba lakini akasema: "Bado uwepo wa Chanongo na Kiemba ndani ya Simba ulikuwa muhimu sana, kila mchezaji ana udhaifu wake kama binadamu, lakini viongozi wanapaswa kukaa na wachezaji kuzungumza nao kujua matatizo yao."
Kiemba alijiunga na Azam kwa mkopo kama Chanongo alivyokwenda Stand United ya Shinyanga.
"Simba haina wachezaji wengi wenye uzoefu, waliopo ni wazuri lakini hakuna umoja wa dhati, bado kuna makundi kwa wachezaji, viongozi waangalie hili kwa kina, ijapokuwa matokeo yanaumiza sana na nimekuwa nikifuatilia Simba kwa karibu," alisema Phiri
"Kwa sasa wasije kufanya kosa la kumfukuza kocha, wakae waangalie wapi kuna tatizo ndani na nje ya timu, bado wana nafasi ya kufanya vizuri bado mechi ni nyingi."
Mzungu amshangaa Chollo
Kopunovic ameshangazwa na tukio la beki mkongwe kuamua kupiga penalti ambayo iliwanyima sare dhidi ya Mbeya City, lakini akatamka kwamba kupoteza mchezo huo ni vizuri kwa sasa kwa sababu itawashtua na kuwarudisha mchezoni kwavile wachezaji walishaanza kujisahau.
"Sawa, sikuwahi kusema nani apige penalti ya kwanza katika mechi zetu, lakini Chollo kupiga penalti lilinishangaza sana kwa kuwa ukiacha mazoezini sikuwahi kumuona akipiga penalti katika mechi lakini sitaki kumlaumu sana," alisema Kopunovic akizungumzia penalti iliyokoswa na Nassor Masoud 'Chollo' na kuipa Mbeya City ushindi wa mabao 2-1.
"Angalia tulivyocheza dakika 30 za mwisho, kwa namna moja nafurahia haya matokeo unajua tangu tuchukue Kombe la Mapinduzi wachezaji wangu walijisahau walikuwa wanajiona wao mastaa wakubwa ni kama wamechukua ubingwa wa ligi, hapa sasa wataamini kuwa safari yao bado ni ndefu."

Tuesday, 27 January 2015

TAARIFA MTANDAO WA FACEBOOK KUPOTEA DUNIANI KWA DAKIKA 40

TAARIFA MTANDAO WA FACEBOOK KUPOTEA DUNIANI KWA DAKIKA 40

Mtandao wa kijamii wa facebook ulikuwa hauingiliki katika maeneo mengi duniani mapema leo kabla ya huduma zake kurudi.
Mamilioni ya watumizi wa mtandao wa facebook walishindwa kuingia katika akaunti zao.
Wateja wake katika mataifa mengine walishindwa hata kutumia hudumu ya Instagram.
Facebook ilisema kuwa wahandisi wake ndio walioababisha tatizo hilo, na kukana madai kwamba kundi moja linalotekeleza uhalifu wa mitandaoni lilihusika.
''Awali watu wengi walikuwa hawawezi kuingia katika akaunti zao za mitandao ya facebook pamoja na huduma ya Instagram'', msemaji wa facebook aliiambia BBC.
''Hili halikuwa shambulizi kutoka kwa watu wengine lakini lilitokea baada ya kufanya mabadiliko ambayo yaliathiri mpangilio wa mfumo wetu''.
Tuliharakisha na kutatua tatizo hilo na sasa huduma zote zimerejelea asilimia 100 kama kawaida
Mitandao hiyo ilitoweka kwa takriban dakika 40 kabla ya kurudi.
Programu ya mtandao unaowaunganisha wapendanao Tinder ambayo hutegemea facebook ili kutoa huduma zake pia iliathiriwa na tataizo hilo.
Kundi moja la uhalifu wa mitandano kwa jina Lizard Squad liliandika ujumbe kwa twitter kuhusu hudumu hiyo kutoweka na kusababisha ripoti kwamba huenda lilihusika.
Kundi hilo limeshtumiwa kwa mashambulizi ya mitandaoni mwishoni mwa mwaka uliopita ambapo michezo ya video ya Sony pamoja na Xbox ilipotea.