Baada ya siku 40: sura ya mtoto wa Diamond na Zari ndio hii imeonyeshwa kwenye picha !
Zimeshatimia siku 40 toka mtoto wa Diamond Platnumz na Zarinah Hassan
azaliwe, anaitwa Tiffah…. ambapo siku hii kubwa ilikumbukwa na nyumbani
kwa Diamond watu mbalimbali wakaalikwa kama ilivyo kwenye utaratibu. Picha zote 3 za juu ni kutoka kwenye Instagram page ya @8020fashions Ustaa
wa Diamond Platnumz na Zari umeshawishi mpaka kampuni kubwa za
kibiashara kuingia mkataba wa malipo kutumia jina na picha za Tiffah
kibiashara ambapo mtoto huyu ambaye ndio kwanza katimiza siku 40 za
kuzaliwa, tayari ni balozi wa maduka ya nguo za watoto Dar es salaam
lakini pia picha yake ya kwanza imeonyeshwa ikiambatana na udhamini wa
benki.
No comments:
Post a Comment